2013-09-10 15:16:29

Papa akutana na walei wawakilishi wa vyama na jumuiya za kikanisa Italy


Jumatatu, Papa alikutana na wawakishi kadhaa wa vyama na jumuiya za kikanisa akiwemo, Rais wa jumuiya ya Uhuisho mpya wa Kiroho, Bwana Salvatore Martinez, Rais wa Chama Katoliki cha Italia , Franco Miano , pia Rais wa jumuiya ya uhuisho wa kiroho katika udugu na upendo, Mateo Caliisi na bibi Michelle Moran, Rais wa Kitaifa kwa jumuiya ya uhuisho mpya wa Roho Mtakatifu. Wote wa Italy .

Papa katika mazungumzo na Salvatore Martinez, Rais wa Jumuiya ya Uhuisho Mpya wa Roho Mtakatifu, aliikumbuka ziara yake ya kichungaji ya kimataifa ya hivi karibuni, Rio de Janeiro, akisema ulikuwa ni mkutano wa Kipentekoste, ambamo walipata nafasi ya kuzungumza, katika muono wa neema mpya katika njia za wokovu. Mkutano ulioweza kuwakutanisha vijana toka pande zote za Dunia , waliofika usikiliza Neno la Mungu na kuliishi katika umoja na mshikamano wa kikanisa. Papa ameonyesha kufurahi kwamba, kuna juhudi nyingi nzuri zinazo fanyika kwa ajili ya Mabadiliko chanya ndani ya Kanisa na dunia, Na hivyo Papa alionyesha ukaribu wake na vikundi hivi vya uamusho katika Kanisa.

Rais Martinez, mara baada ya kukutana na Papa, aliwasilisha zawadi zilizoandaliwa na vijana wafungwa wa zamani , ambao kwa sasa hujishughulisha na vijana ambao bado kifungoni, katika Kituo cha Malezi Bora cha Polo, Mario na Luigi Sturzo, na pia zawadi kutoka wa wahamiaji wa Lampedusa ambao kwa sasa wamehamishiwa Sicily. Ni zawadi zilizotengenezwa kwa udogo wa kauri zilizosindikwa katika kituo hicho cha Sturzo.

Na pia katika mazungumzo yao, walifanya mapitio katika shughuli zinazo fanywa na jumuiya kwa manufaa ya wahamiaji katika mji wa Lampedusa, wafungwa na kituo cha Malezi cha Sturzo, watoto na familia katika Moldavia na kisha Kituo cha Kimataifa cha Familia ya Nazareti, walicho kabidhiwa jumuiya ya Uhuisho Mpya wa Kiroho na ambacho Baba Mtakatifu tayari anakifahamu. Papa alionyesha kuvutiwa na shughuli za Kiroho , majiundo mpya ya kiroho na Uinjilishaji wa RNS , ambamo wanajumuiya wake wako tayari kupeleka Neno la Mungu katika mataifa mengine.

Na pia walizungumzia Ukristu barani ulaya hasa haja ya uinjilishaji mpya nchini Italia, na udumishaji wa juhudi za vijana na familia. Na pia waliunga mkono juhudi za mradi , unaojulikana kama mraba 10 10 wa Amri za Mungu , ambao utaanza rasmi Septemba 21, huko Palermo , ambamo Baba Mtakatifu, atatoa ujumbe wake kupitia matangazo ya video, na utaweza kusikika katika miji kadhaa.

Baba Mtakatifu ameomba kwa unyenyekevu mkubwa, daima kumkumbuka katika maombi yao , kama hakikisho maalum na ukaribu wake wa kichungaji kwa jumuiya na pia kwa ajili ya utendaji wa shughuli katika mipango ya baadaye na mipango yake mwenyewe binafsi.

Jumuiya ya uhuisho mpya wa Roho Mtaktifu RnS, ina wanajumuia zaidi ya 200,0000, wanaounda vikundi zaidi ya 1,900, hapa Italia.








All the contents on this site are copyrighted ©.