2013-09-05 14:31:53

Wito wa Maaskofu Katoliki wa Ghana kwa wanasiasa


Maaskofu Katoliki nchini Ghana wameitaka serikali na vyama vya upinzani , kufanyakazi kwa ushirikiano na kutengeneza mazingira yanayofaa, vijana kupata ajira, kuepusha matendo maovu, rushwa na ubadhilifu, ubabe wa kisiasa au kidini usiokuwa na kiasi na kuenea kwa maradhi ya zinaa katika taifa pendwa la Ghana.

Tamko la Maaskofu la Jumatatu, linahimiza wananchi wa Ghana , kujenga moyo wa mashauriano na maridhiano kwa ajili ya uwepo wa mshikamano wa kitaifa kwenye uwajibikaji wa wote katika kutatua kero na matatizo yanayo jirudia mara kwa mara, katika jamii.

Hati ya MAaskofu imetiwa sahihi na Askofu Mkuu Joseph Osei Bonsu, Rais wa Baraza la Maaskofu Katoliki Ghana(CBCG). Ni tamko linalo onyesha uwajibikaji katika vipengere nyeti vinavyohitajika kufanyiwa mapitio ya kina hasa katika taratibu za uchaguzi na marekebisho katika Kaatiba na changamoto zingine ngumu zinazohusiana na taratibu za uchaguzi, nchini humo.

Maaskofu wanatazamia Waghana wote wataweza kuitikia ombi la Maaskofu kwa moyo wa hekima na busara , bila ya kujali hadhi yao kisiasa, kiitikadi, kidini au asili za ukabila. Ni kufuta kutofautiana kwa nyuma na kusonga mbele na sura mpya ya umoja na mshikamano wa kitaifa kwa ajili ya kudumisha amani Ghana.








All the contents on this site are copyrighted ©.