2013-08-29 15:20:11

Mitandao ya kijamii: Milango ya ukweli na imani, uwanja mpya wa uinjilishaji


Baraza la Maaskofu Katoliki Afrika Kusini litaadhimisha Jumapili ya mawasiliano ya kijamii siku ya Jumapili ya tarehe 1 Septemba 2013. Mada ya maadhimisho hayo itakuwa Mitandao ya kijamii: Milango ya ukweli na imani, uwanja mpya wa uinjilishaji.

Maaskofi Katoliki nchini Afrika Kusini wamechangamotishwa na mada ya siku ya mawasiliano duniani juu ya mitandao ya kijamii iliyotolewa na Baba Mtakatifu mstaafu Benedikto wa kumi na sita. Maaskofu hawa wa Afrika Kusini wamewaandikia barua waumini wote nchini humo kushiriki kwenye maadhimisho ya siku ya mawasiliano nchini humo hapo siku ya Jumapili (01.09.2013).

Maaskofu hao wamesema kwamba Baba Mtakatifu anawaalika wote kutumia mitandao ya kijamii kwa ajili ya uinjilishaji na hivyo jamii ya waumini haina budi kuandaa washa na semina kwa ajili ya mafunzo juu ya utumiaji muafaka wa mitandao hiyo.

Makanisa na Parokia hayana budi kuchagua mitandao inayofaa na kuitumia kwa ajili ya manufaa ya jamii kwa ujumla, wakizingatia maswala ya kisheria, kimaadili na kiroho hata katika utumiaji huo ili kuweza kufanya uinjilishaji muafaka kwa kizazi kipya.

Maaskofu hawa pia wamewachangamotisha waumini kuchambua njia wanazotumia katika kuwasiliana kwenye maparokia na kuhakikisha kupyaisha njia zote za mawasiliano ili kuweza kuliendeleza kanisa nchini humo.











All the contents on this site are copyrighted ©.