2013-08-29 15:17:56

Italia kutoingilia mgogoro wa Syria


Italia haitashiriki kwenye mashambulizi ya kisilaha dhidi ya Syria ikiwa Umoja wa Mataifa hautahusika kwenye mashambulizi hayo. Haya yamesemwa na Waziri Mkuu wa Italia Bw. Enrico Letta kwenye mahojiano na Radio Anchiā€™io yenye kurushia matangazo yake mjini Roma. Hata hivyo, amesema Waziri Mkuu Letta kwamba nchi yake inalaani vikali vitendo vya kikatili vinavyotekelezwa na serikali ya rais Bashar Assad wa Syria dhidi ya wananchi wa Syria.

Hapo awali rais Barrack Obama wa Marekani alinukuliwa na Shirika la Habari la AP akisema kwamba nchi yake imethibitisha kwamba serikali ya Assad ndiyo iliyohusika na mashambulizi ya kikemikali ya hivi karibuni yaliyosababisha vifo vya watu karibiya 100 nchini Syria. Marekani inasema kuna haja ya jumuiya ya kimataifa kuingilia kati ili kuithibiti serikali ya Bashar Assad dhidi ya kutumia silaha za kemikali kwani shambulizi la aina hii lina athari ya kimataifa.

Waziri mkuu wa Italia Bw. Enrico Letta hata hivyo ameiomba jumuiya ya kimataifa kuchukua tahadhari kubwa katika kuingilia kati mzozo wa Syria. Italia na mataifa mengine ya Ulaya yanachukua tahadhari hiyo kwani bado kuna utata juu ya nani hasa kaagiza utumiaji wa mashambulizi kwa kutumia silaha za kikemikali nchini Syria.

Baba Mtakatifu Francisko kwenye ujumbe wake katika mtandao wa kijamii wa Twitter siku ya Alhamisi anasema kwamba Upendo wa Mungu sio kitu cha hewani, ila ni kitu chenye jina na sura: Yesu Kristo. Hivyo ni mwaliko kwa jumuiya ya kimataifa kuona sura na jina la Yesu Kristo ndani ya watu wote wanaoteseka na kuchukua hatua ambazo zitaisadia nchi ya Misri kumaliza vurugu na kinzani za kivita zinazoendelea nchini humo,

Jumuiya ya kimataifa inapoamua kuingilia kati mgogoro wa Syria, inapaswa kuchukua tahadhari kubwa na kuonyesha upendo mkuu kwa wananchi wa Syria wasio na hatia na wanaoendelea kuteseka kwani wanajikuta katikati ya vita na kinzani wasichokielewa.









All the contents on this site are copyrighted ©.