Jumapili
wakati wa adhuhuri, akiongoza sala ya Malaika wa Bwana mbele ya umati mkubwa wa mahujaji
na wageni waliofurika katika Uwanja wa Kanisa kuu la Mtakatifu Petro hapa Vatican,
aliutumia muda huo, kuomba amani kwa taifa la Syria, ambako watu wanaendelea kuishi
katika hali za vitisho vya ukatili mkubwa wa machafuko ya wenyewe kwa wenyewe, na
hasa mwelekeo wa kufumka wa wimbi jipya la vita. Papa alitoa wito huo huku akionyesha kuguswa na hali hiyo ya mateso na wasiwasi
mkubwa kwa watu wa Syria, ambako katika kipindi hiki cha miaka miwili na nusu ya
vita vya wenyewe kwa wenyewe, zaidi ya watu 100 elfu kati yao elfu 7 wakiwa watoto
wamepoteza maisha yao. Na zaidi ya millioni 4 kwa wakati huu wanaishi kama wakimbizi
ndani ya nchi yao na nje ya nchi. Katika hali hiyo ya masikito Papa alisema,” kwa mara nyingine, nalazimika
kupaza sauti yangu nikiwaomba wote wale wanao husika na ghasia hizi,wasikilize kilio
cha watu wasiokuwa na hatia na wasitishe ukatili huo unaoendelea kutesa na kudhulumu
watu kwa ghasia za mapigano na hasa matumizi ya silaha kali, kushambuliana ndugu
kwa ndugu, kama inavyo elezwa na kushuhudiwa katika vyombo vya habari. |
Papa ameasa, kuongezeka kwa ghasia za wenyewe kwa wenyewe
hakuwezi kutoa jibu la uwepo wa matumaini katika mustakhabali wa taifa , njia pekee
ya kupata ufumbuzi katika tofauti zao ni kupitia njia ya majadiliano , mmoja akisikiliza
uzito wa hoja ya mwingine katika hali ya amani na maridhiano, na kuona jinsi wanavyoweza
kusawazisha tofauti hizo kwa makubaliano. Papa alionyesha ukaribu wake kupitia sala na msaada wa kihali unaotolewa
daima, na vyombo vya misaada vya Kanisa kwa wahanga wote wa vita hii, na kwamba,
anafuatilia kwa makini kinachoendelea Syria na hasa hali ya wakimbizi na watoto, na
daima anawasihi wasikate tamaa bali waendelee kudumu katika tumaini la amani Na aliigeukia jumuiya ya Kimataifa, akiitaka
ionyeshe uwajibikaji zaidi katika juhudi za kusitisha ukatili unaoendelea Syria ,
na wakati huohuo, itoe msaada si tu wa kihali lakini hawa katika upatikanaji wa jawabu
sahihi la kusitiza vita inavyoendelea kufanya uharibifu na mauaji. Na mwisho alitoa mwaliko kwa watu wote
kutolea sala zao kwa Malkia wa amani . Yesu ni njia
pekee ya wokovu |
All the contents on this site are copyrighted ©. |