2013-08-26 13:56:47

Ni vigumu kunyamalia kilio cha watoto wahanga Syria Mons. Zenari


Akihojiwa na Redio Vatican juu ya vitendo vya kutisha vinavyoendelea Syria, Mjumbe wa Papa wa Damscus, Askofu Mkuu Mario Zenari, anasema, katika siku za hivi karibuni , ambako kumekuwa na utendaji wa kinyama kwa watoto wasiokuwa na hatia, ni vigumu kunyamalia kilio cha watoto hao, kinachoililia mbingu na jumuiya ya kimataifa, kuona mateso na mahangaiko yao.
Ameserma ni wazi, katika siku hizi, wanainua zaidi sauti katika sala kuomba jumuiya ya kimataifa iwajibike zaidi,na kutumia busara zaidi, ili kupata jawabu linalo faa kusitisha kipeo hiki cha syria. Jumuiya ya Kimataifa inapaswa kutoa jibu haraka lakini makini, ili uharifu na unyama huu kamwe usipate kujirudia Syria,
Na akijibu swali juu ya utumiaji wa silaha za kemikali, amesema, jumuiya ya kimataifa inapaswa kuthibitsha ukweli wa taarifa zinazotolewa kwamba, silaha za kemikali zimetumika na pia kuingilia kati kuhakikisha utawala mahalia, unatoa ushirikiano wa kutosha kwa hoja hii, pia kwa pande zote zinazo husika katika mzozo huo.

Askofu Zenawi, ameitaka jumuiya ya Kimataifa itende kwa haraka, kufanikisha maridhiano ya kitaifa kwa ajili ya kukomesha machafuko hayo.







All the contents on this site are copyrighted ©.