Jitokezeni kwa wingi ili kuombea amani duniani hapo tarehe 21 Septemba 2013
Baraza la Makanisa Ulimwengu linawaalika Makanisa wanachama kuhakikisha kwamba, yanashiriki
kikamilifu katika Siku ya Kuombea Amani Kimataifa, itakayoadhimishwa hapo tarehe 21
Septemba 2013. Kauli mbiu inayoongoza Maadhimisho haya ni "Mungu wa uhai, tuongoze
katika haki na amani".
Baraza la Makanisa Ulimwengu litafanya kumbu kumbu
hii kwa kushirikiana na Umoja wa Mataifa. Katika miezi ya hivi karibuni, kumekuwepo
na matukio sehemu mbali mbali za dunia yanayoonesha uvunjifu wa misingi ya haki, amani,
upendo na mshikamano kati ya watu; mambo ambayo yanaendelea kusababisha mateso na
mahangaiko makubwa kwa watu.
Sala ni silaha madhubuti katika kupambana na
malimwengu. Siku ya kuombea amani kimataifa ilianzishwa kunako mwaka 2004 baada ya
Katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa kukubaliana na kimsingi na ombi lililotolewa na Baraza
la Makanisa Ulimwenguni.