2013-08-24 11:14:25

Jifunzeni kutoka kwa Papa Francisko katika kuwahudumia watu wenu!


Askofu mkuu Joseph Coutts wa Jimbo kuu la Karachi na Rais wa Baraza la Maaskofu Katoliki Pakistan anasema, unyenyekevu unaooneshwa na Baba Mtakatifu Francisko ni amana kubwa inayoweza kusaidia kuleta mabadiliko katika maisha na utume wa Kanisa na Jamii katika ujumla wake.

Askofu mkuu Coutts ameyasema hayo hivi karibuni alipokuwa anazungumza na wanataaluma, wakurugenzi pamoja na viongozi wa kisiasa nchini Pakistan. Anasema, viongozi mbali mbali wanayo mengi ya kujifunza kutoka kwa Baba Mtakatifu Francisko katika mchakato wa kukuza na kudumisha majadiliano ya kidini na kiekumene, ili kujenga dunia inayosimikwa katika misingi ya haki, amani na upatanisho wa kweli, vielelezo msingi katika maisha ya Mtakatifu Francisko wa Assisi.

Baba Mtakatifu ni kiongozi anayeonesha dira kwamba, uongozi ni huduma kwa ajili ya maskini na wote wanaosukumizwa pembezoni mwa Jamii. Uongozi ni kielelezo cha upendo na mwaliko wa kujenga utamaduni wa kusikiliza na kuwajali wengine katika shida na mahangaiko yao ya ndani.

Ikiwa kama viongozi katika medani mbali mbali za maisha watajifunza kusikiliza na kuhudumia kwa makini, jamii nyingi zinaweza kuonja mabadiliko ya kweli kutoka katika undani mwao!







All the contents on this site are copyrighted ©.