Rais Robert Mugabe wa Zimbabwe, Alhamisi amekula kiapo cha kuwaongoza wananchi wa
Zimbabwe kwa kipindi kingine cha miaka mitano. Sherehe hii imeongozwa na Bwana Godfrey
Chidyausiku, Jaji mkuu wa Zimbabwe na kuhudhuriwa na umati mkubwa wa wananchi wa Zimbabwe.
Rais
Mugabe aliwaongoza wananchi wa Zimbabwe kujipatia uhuru wao kunako mwaka 1980, akaapa
kutetea masilahi na haki za wananchi wanyonge nchini Zimbabwe.
Katika sherehe
za kuapishwa kwa Rais Mugabe, Chama Kikuu cha Upinzani, hakikuhudhuria kwa madai kwamba,
uchaguzi hakuwa huru wala wa haki na kwamba, kulikuwa na ukiukwaji mkubwa wa kanuni
za uchaguzi, tuhuma ambazo zimetupiliwa mbali na Mahakama kuu ya Zimbabwe na hivyo
kuhalalisha ushindi wa Rais Mugabe katika uchaguzi mkuu uliofanyika hapo tarehe 31
Julai 2013.
Sherehe hizi zimehudhuriwa na viongozi kadhaa kutoka katika nchi
za SADC