Baraza la Maaskofu Katoliki Misri linasema kwamba, kuna Makanisa 58 na Majengo kadhaa
ya Taasisi za Makanisa yamechomwa moto na kuharibiwa vibaya. Kati ya Makanisa 58,
yaliyochomwa moto, kuna Makanisa 14 ya Kanisa Katoliki. Makanisa haya yamechomwa moto
katika maeneo: Al Minya na Assiut yanayokaliwa na Waislam wenye imani kali.
Baraza
la Maaskofu Katoliki Misri linasema kwamba, hii si vita kati ya Waislam na Wakristo,
kwani kuna raia wema wa dini zote walioshiriki kusaidia kuzima moto kwa Makanisa yaliyokuwa
yanateketea. Kanisa linasema hii si vita ya wenyewe kwa wenyewe bali ni vita dhidi
ya vitendo vya kigaidi vinavyofanywa na baadhi ya wananchi wa Misri na waamini wenye
misimamo mikali ya kiimani.