Onesheni mshikamano wa upendo kwa watoto wanokufa kwa njaa!
Baba Mtakatifu Francisko katika mafundisho yake anaendelea kuwahimiza waamini na watu
wote wenye mapenzi mema kuondokana na utandawazi usiojali wala kuguswa na mahangaiko
ya jirani na badala yake kuanza mchakato wa mshikamano wa upendo na udugu, kwani wote
ni watoto wa Mungu, licha ya tofauti zao mbali mbali.
Baba Mtakatifu Francisko
katika ujumbe wake kwa watumiaji wa mitandao ya kijamii al maarufu kama twitter anasema,
haiwezekani kupata usingizi mnono wakati ambapo kuna maelfu ya watoto wanaofariki
dunia kutokana na baa la njaa na utapiamlo wala wazee ambao hawana huduma za afya.
Wachunguzi
wa masuala ya mawasiliano ya kijamii wanasema kwamba, Baba Mtakatifu Francsiko kwa
sasa anawafuasi wapatao millioni 8 ambao wamejisajili kwenye akaunti yake ya twitter.