Monsinyo Jean Marie Speich ateuliwa kuwa Balozi wa Vatican nchini Ghana
Baba Mtakatifu Francisko amemteua Monsinyo Jean Marie Speich kuwa Balozi Mpya wa Vatican
nchini Ghana pamoja na kumpandisha hadhi ya kuwa ni Askofu mkuu.
Kabla ya
uteuzi huu Askofu mkuu mteule Jean Marie Speich alikuwa ni mshauri wa mambo ya nje
na ushirikiano wa kimatifa katika Sekretarieti ya Vatican.