MDC yafungua kesi mahakamani kupinga matokeo ya uchaguzi mkuu Zimbabwe
Chama cha Upinzani cha MDC kinachoongozwa na Bwana Morgan Tsvangirai, mwishoni mwa
juma, kimefungua kesi ya kupinga matokeo ya uchaguzi mkuu kwenye Mahakama kuu nchini
Zimbabwe.
MDC kimeamua kufungua kesi Mahakama Kuu baada ya Tume ya uchaguzi
nchini Zimbabwe kushindwa kutoa majibu muafaka ya mashaka yaliyooneshwa na Chama hiki
pamoja na baadhi ya waangalizi wa kimataifa kusema kwamba, kulikuwa na kasoro katika
uchaguzi mkuu uliofanyika nchini Zimbabwe, hapo tarehe 31 Julai 2013 na Rais Robert
Mugabe kuibuka kidedea.