Serikali ya Afrika ya Kusini, Jumapili iliyopita katika taarifa yake kwa vyombo vya
habari inasema kwamba, hali ya afya ya Mzee Nelson Mandela, aliyekuwa Rais wa Afrika
ya Kusini inaendelea kuboreka kwa kiwango kidogo sana.
Mzee Madiba mwenye
umri wa miaka 95 anaendelea kupata matibabu mjini Pretoria kwa muda wa miezi miwili
kwa sasa. Watu wengi bado wanaendelea kumkumbuka na kumwombea katika sala na dua zao.