2013-08-10 09:53:05

Mfuko wa Uwezo Kenya, unapania kutoa fursa za ajira kwa vijana


Serikali ya Kenya imeamua kutoa mikopo isiyokuwa na riba kwa wajasiriamali vijana na wasichana kama sehemu ya mchakato wa kupambana na ukosefu wa ajira pamoja na umaskini miongoni mwa vijana. Serikali imetenga kiasi cha shilingi za Kenya billioni sita zitakazotolewa kwenye Mfuko wa Uwezo.

Lengo hili limetangazwa hivi karibuni na Makamu wa Rais wa Kenya Bwana William Ruto anayekazia kwamba, mfuko wa uwezo utaanza kutoa mikopo isiyokuwa na riba kuanzia mwezi Septemba baada ya kupokea na kupitisha maombi ya vijana kutoka sehemu mbali mbali nchini Kenya.

Vijana watapaswa kuitumia fedha hii kwani watalazimika kuiridisha kadiri ya mkataba. Wale watakaofanikiwa watakuwa na nafasi nzuri ya kupewa tena mkopo huo.







All the contents on this site are copyrighted ©.