Simameni kidete kulinda na kutetea zawadi ya maisha dhidi ya vita!
Kumbukumbu ya Miaka 68 tangu miji ya Hiroshima na Nagasaki ilipolipuliwa kwa mabomu
ya atomic ni kielelezo kwamba, hata leo hii, dunia bado kuna hofu kubwa ya maafa yanayoweza
kujitokeza kutokana na umilikaji wa silaha za kinyuklia. Hii ni changamoto kwanza
kabisa ya kuhakikisha kwamba, watu wanasimama kidete kulinda na kutetea zawadi ya
maisha, ili maafa ya Hiroshima na Nagasaki yasijirudie tena duniani.
Dr. Olav
Fykse Tveit, Katibu mkuu wa Baraza la Makanisa Ulimwenguni anasema, Maadhimisho ya
Mkutano mkuu wa kumi wa Baraza la Makanisa Ulimwenguni utakaofanyika huko Korea na
ya Kusini, itakuwa ni fursa ya kuangalia tena ukakasi wa vita baridi unaoendelea kujitokeza
katika Jumuiya ya Kimataifa; mataifa bado yanatishia kutumia silaha za nyuklia katika
mapambano.
Dr. Tveit anasema watu wanahitaji kuishi katika amani na utulivu
na wala si kuendelea kuwa na wasi wasi wa mashambulizi ya silaha za kinyuklia. Amani
iwe ni jiwe la msingi katika mahusiano ya kimataifa. Wazee walionusurika kutokana
na maafa ya Hiroshima na Nagasaki, wawe ni kielelezo cha matumaini ya dunia isiyokuwa
na vitisho vya vita. Ni changamoto ya kulinda na kutetea zawadi ya maisha ambayo ni
kwa ajili ya wote!