2013-08-05 10:31:39

Kumbu kumbu ya Mtaguso wa Efeso uliofanyika kunako mwaka 431


Baba Mtakatifu Francisko mara baada ya Sala ya Malaika wa Bwana, Jumapili tarehe 4 Agosti 2013 alitambua uwepo wa makundi mbali mbali na umati mkubwa wa vijana.

Ametumia fursa hii kuwakumbuka kwa namna ya pekee Maparoko wote kutoka sehemu mbali mbali za dunia walipokuwa wanaadhimisha Kumbu kumbu ya Mtakatifu Yohane Maria Vianney, Msimamizi wa Maparoko. Baba Mtakatifu anasema, anaungana nao katika sala na upendo wa shughuli za kichungaji.

Baba Mtakatifu pia amekumbushia kuhusu Siku kuu ya Kutabarukiwa kwa Kanisa la Bikira Maria Mkuu, lililoko mjini Roma, lililojengwa kwa heshima ya Mama wa Mungu mara baada ya Mtaguso wa Efeso, uliofanyika kunako mwaka 431, hapo Kanisa likamtangaza Bikira Maria kuwa ni "Theotokos" yaani Mama wa Mungu. Baba Mtakatifu Francisko, aliwaalika waamini kusali kwa pamoja salam Maria, kwa ajili ya kumbu kumbu ya Bikira Maria afya ya Warumi.







All the contents on this site are copyrighted ©.