Jaji Francis S. K. Mutungi ateuliwa kuwa ni Msajili mpya wa Vyama vya Siasa Tanzania
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete amemteua
Mheshimiwa Jaji Francis S.K.Mutungi kuwa Msajili wa Vyama vya Siasa. Taarifa iliyotolewa
Dar Es Salaam Jumatatu, Agosti 5, 2013, na kutiwa saini na Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi
Ombeni Sefue imesema kuwa uteuzi huo ulianza Ijumaa iliyopita Agosti 2, 2013.
Jaji
Mutungi anachukua nafasi iliyoachwa wazi na aliyekuwa Msajili wa Vyama vya Siasa,
Mhe. John Tendwa ambaye amestaafu Utumishi wa Umma kwa mujibu wa sheria. Kabla ya
uteuzi huo, Jaji Mutungi alikuwa Jaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Dodoma.