2013-08-05 07:38:03

Baa la njaa nchini Swaziland na athari zake


Athari ya baa la njaa ni kubwa zaidi kuliko thata ukosefu wa nguvu mwilini kutokana na kutopata chakula cha kutosha na chenye madini muhimu ya kuulisha mwili. Athari hizi hujionesha hasa kwenye sekta za elimu na afya ambapo imebainika kwamba, watoto wanaokosa chakula na lishe bora hupata shida ya kuelewa vyema masomo shuleni, na hatimaye, kama watu wazima wanaweza kujikuta wakitupwa pembezoni mwa jamii kwa kutoweza kujimudu kimaisha kama matokeo ya moja kwa moja ya baa la njaa. RealAudioMP3

Haya yamejiri kwenye taarifa ya utafiti wa serikali ya Swaziland iliyowezeshwa na msaada kutoka Shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Chakula Duniani, (WFP).

Utafiti huo pia unabainisha kwamba, hata uchumi wa Swaziland unaathirika kwa kiasi kikubwa, kwani, baa la njaa linasababisha upungufu wa Pato Ghafi la Taifa, kwa asilimia 3.1% ambayo inaweza kulinganishwa na dola za kimarekani milioni 92. Pia kama matokeo ya moja kwa moja ya ukosefu wa chakula, watoto asilimia 12% wenye umri wa kuwa shuleni hawamalizi masomo yao, pia asilimia 40% ya wafanyakazi nchini humo wameathiriwa na magonjwa yanayotokana na ukosefu wa chakula na lishe bora walipokuwa watoto.

Utafiti huo pia umebainisha kuwa, baa la njaa huwaathiri watoto 46,000 kati ya watoto 156,000 walio chini ya umri wa miaka 5, au watoto watatu kati ya kila watoto 5 wanaozaliwa. Zaidi ya hayo, ukosefu wa huduma muhimu unachangia kuongeza kwa athari hizo, kwani asilimia 69% za kesi za utapiamlo hazipati matibabu.

Kwenye miezi ya hivi karibuni, Swaziland, ambayo ndiyo nchi ya pekee Barani Afrika iliyo na mfumo wa utawala wa kifalme, imeshuhudia upinzani kutoka makundi yanayo tetea haki msingi za binadamu na utawala wa kidemokrasia yanayotaka uhuru wa kujieleza na haki za kibinadamu. Swaziland inasisitiza kufanya uchaguzi wa wabunge wake kati ya Mwezi Agosti na Septemba, 2013 ijapokuwa upinzani umetishia kuugomea uchaguzi huo.









All the contents on this site are copyrighted ©.