Kardinali Leonardo Sandri, Mwenyekiti wa Baraza la Kipapa la Makanisa ya Mashariki
anaungana na viongozi wa Mashirika ya Makanisa ya Mashariki kuonesha moyo wake wa
mshikamano na Wayesuit wote kutokana na wasi wasi wa kupotea katika mazingira tata
Padre Paolo Dall'Oglio.
Baraza la Kipapa bado linaendelea kusali na kuwambuka
pia Maaskofu wawili na Mapadre wawili kutoka Mashariki waliotekwa nyara hadi sasa
hawajulikani mahali walipo. Kardinali Sandri anasema, anawakumbuka hata wananchi wengine
wote wa Syria na wageni ambao wanaendelea kupotea katika mazingira tata. Kardinali
Sandri anaendelea kusali ili amani iweze kurejea tena huko Syria na Mashariki ya Kati.