Silvio Berlusconi afungwa jela miaka 4 kwa kukwepa kulipa kodi stahiki na kujihusisha
na vitendo vya rushwa!
Mahakama kuu ya Italia siku ya Alhamisi, tarehe Mosi Agosti, 2013 imemtia hatiani
Bwana Silvio Berlusconi ambaye amewahi kuwa Waziri mkuu wa Italia na mfanyabiashara
maarufu nchini Italia kwa kosa la kukwepa kulipa kodi stahiki pamoja na kujihusisha
na rushwa.
Kwa makosa haya makuu, Bwana Berlusconi amehukumiwa miaka 4 kwenda
jela. Mahakama kuu imetoa amri kwa Mahakama ya rufaa kuangalia jinsi ya kurekebisha
utekelezaji wa hukumu iliyokuwa inamnyima haki ya kushiriki katika masuala ya kisiasa
kwa miaka mitano. Kwa sasa Bwana Berluscon ataendelea kuwa ni Seneti na Mwenyekiti
wa Chama chake cha PDL. Lakini kutokana na umri wake wa miaka 76 anaweza kutumikia
kifungo cha nje au kutoa huduma kwa jamii. Bwana Berluscon anasema yeye anatamani
kwenda jela.
Kwa hukumu hii, Serikali ya Umoja wa Kitaifa nchini Italia iko
mashakani, lakini Rais Giorgio Napolitano wa Italia amewataka wanasiasa kudumisha
utawala wa sheria na utulivu kwa ajili ya mafao ya wananchi wa Italia hasa wakati
huu ambapo hali bado ni tete katika ujumla wake.