Fuateni sheria, kanuni na miongozo ya Liturujia ya Kanisa
Baba Mtakatifu Francisko anatarajia hivi karibuni kuchagua kiongozi wa kitume atakayefuatilia
masuala ya: maisha, uongozi, utume na liturujia inayoadhimishwa na Shirika la Ndugu
wadogo wa Mtakatifu Francisko wa Bikira Maria Mkingiwa Dhambi ya Asili.
Ufafanuzi
huu umetolewa na Padre Federico Lombardi, Msemaji mkuu wa Vatican na kukazia kwamba,
Baba Mtakatifu anawataka Watawa hawa kuadhimisha Mafumbo ya Kanisa kadiri ya sheria
na kanuni za Kanisa kama zilivofafanuliwa na Baba Mtakatifu mstaafu Benedikto wa kumi
na sita. Hakuna sababu ya kuwa na mkanganyo katika Maadhimisho ya Ibada ya Misa Takatifu
wala kuwa na kinzani katika masuala haya. Sheria, kanuni na taratibu zinapaswa kufuatwa
kikamilifu.