2013-07-31 09:42:49

Makanisa yanapania kuendelea kuwasaidia Wakristo wanaoishi katika Nchi Takatifu


Kuna umuhimu wa kuisaidia Nchi Takatifu ili iendelee kutimiza majukumu yake ya kutoa huduma ya upendo kwa watu wanaoishi pembezoni mwa jamii na wahitaji. Haya yamesemwa hivi karibuni na Askofu Mkuu Justin Welby, wa Jimbo kuu la Cantebury ambaye pia ni Kiongozi mkuu wa Kanisa Anglikani Duniani, alipokutana na wawakilishi wa kundi la Marafiki wa Nchi Takatifu.

Hili ni kundi la kiekumene ambalo lililoundwa kunako mwaka 2009, lina makao yake Makuu nchini Uingereza na lina malengo ya kuwasaidia Wakristo wanaoishi katika Nchi Takatifu. Wakati wa mkutano huo, Askofu Mkuu Welby alikubali kuchukua nafasi iliyoachwa wazi na Askofu mkuu mstaafu Rowan Williams wa Jimbo kuu la Canterbury, kama mmoja wa wafadhili wa nchi Takatifu.
Wafadhili wengine ni pamoja na Askofu mkuu Vincent Gerard Nichols Rais wa Baraza la Maaskofu Katoliki Uingereza na wengi wa marafiki wa Nchi Takatifu ni waamini wa Kanisa la Kiangalikiani nchini Uingereza. Wafadhili hawa pia hutumia muda wao kuwaombea Wakristo wanaoishi katika Nchi Takatifu na kupanga hija za kwenda kwenye maeneo matakatifu nchini humo.








All the contents on this site are copyrighted ©.