Baada ya vita, madhulumu na nyanyaso kutulia, mikakati inafanywa ili kufanya ukarabati
mkubwa Afrika ya Kati
Shirika la Kipapa la Msaada kwa Makanisa hitaji linasema kwamba, tangu Jamhuri ya
Watu wa Afrika ya Kati ilipoingia kwenye vita, kinzani na migogoro ya kijamii; watu
zaidi ya 400 wameuwawa kikatili; wanawake na wasichana wengi wamenyanyaswa na kudhulumiwa
utu na heshima yao. Kuna wananchi wengi ambao wamelazimika kuyakimbia na kuyahama
makazi yao kwa kuhofia usalama wa maisha na mali zao.
Katika mazingira kama
haya, Majimbo 4 ya Kanisa Katoliki yamejikuta kwamba, yamepoteza walau asilimia 50%
ya rasilimali yake, kumbe yanapaswa kusaidiwa kuanza upya. Shirika la Kipapa laMsaada
kwa Makanisa hitaji limetenga fungu maalum kwa ajili ya ukarabati wa Makanisa na nyumba
za Mapadre kwa majimbo manne ya Kanisa Katoliki nchini Afrika ya Kati.
Makanisa
mengi yameporwa na kunajisiwa, hali ambayo kwa sasa inakwamisha maisha na utume wa
Kanisa Majimboni humo. Haya yamo kwenye taarifa iliyoandikwa na Askofu Juan Josè Aguirre
wa Jimbo Katoliki la Bangassou, Jamhuri ya Watu wa Afrika ya Kati.