Baba Mtakatifu Francisko katika ujumbe wake kwa watumiaji wa mitandao ya kijamii,
anapenda kuwashukuru wote kwa kufanikisha Maadhimisho ya Siku ya 28 ya Vijana Duniani
kwa Mwaka 2013 huko Rio de Janeiro. Anawaaomba waamini na watu wenye mapenzi mema
kumkumbuka katika sala na majitoleo yao.
Itakumbukwa kwamba, Maadhimisho ya
Siku ya 29 ya Vijana Duniani kwa Mwaka 2016 yatafanyika Jimbo kuu la Cracovia, Poland.
Wenyeji wa Maadhimisho haya wanasema, Poland, kutawaka moto hasa wakati huu ambapo
Kanisa linaendelea kujiandaa kwa ajili ya kumtangaza kuwa Mtakatifu Mwenyeheri Yohane
Paulo wa Pili.