Ijumaa, tarehe 26 Julai 2013, Baba Mtakatifu ataianza siku hii kwa Ibada ya Misa Takatifu
na baadaye atashiriki katika kuwaungamisha baadhi ya vijana watakaoshiriki katika
Maadhimisho ya Siku ya Vijana Duniani. Tukio hili linafanyika kwenye Uwanja wa Quinta
da Boa.
Atasalimiana
na baadhi ya vijana wanaotumikia adhabu yao gerezani na mchana atasali na vijana Sala
ya Malaika wa Bwana. Mchana atapata fursa ya kukutana na kuzungumza na Kamati ya Maandalizi
ya Siku ya Vijana na Wafadhili. Siku hii itapambwa kwa vijana kupata chakula cha mchana
na Baba Mtakatifu Francisko. Jioni vijana watashiriki pamoja na Baba Mtakatifu kuadhimisha
Njia ya Msalaba kwenye ufuko wa Copacabana.