Alhamisi, tarehe 25 Julai 2013, Baba Mtakatifu ataanza siku kwa kuadhimisha Ibada
ya Misa Takatifu kwenye makazi yake ya muda hapo Sumarè mjini Rio de Janeiro. Asubuhi
atakaribishwa na kupewa ufunguo wa mji wa Rio de Janeiro pamoja na kubariki bendera
za Olympic.
Atatembelea
Jumuiya ya Varginha na baadaye jioni, hapo shughuli ya kuwakaribisha vijana kutoka
sehemu mbali mbali za dunia, itaanza kucharuka, kiashilio cha Ufunguzi wa Maadhimisho
ya Siku ya Vijana Duniani kwa Mwaka 2013. Shughuli hii itafanyika kwenye ufukwe maarufu
wa Copacabana ulioko mjini Rio de Janeiro.