Maadhimisho ya Siku ya Vijana Dunani yajenge na kuimarisha imani, upendo na mshikamano
wa kidugu!
Kardinali Tarcisio Bertone, Katibu mkuu wa Vatican, katika Maadhimisho ya Siku ya
Vijana Duniani, ametoa medali ya kumbu kumbu ya hija ya kwanza ya kichungaji kufanywa
na Baba Mtakatifu Francisko, tukio ambalo limehudhuriwa na viongozi wa Kanisa, Serikali
na umati mkubwa wa vijana.
Kardinali Bertone, amewapongeza wale wote walioshughulika
kuandaa medali hizi kwa ajili ya kumbu kumbu ya tukio hili la kiimani, ambalo limewakusanya
vijana kutoka sehemu mbali mbali za dunia. Medali inamwonesha jinsi ambavyo Baba Mtakatifu
Francisko alivyo karibu zaidi na watu. Medali hizi ziwasaidie waamini na wote wenye
mapenzi mema kufurahia zawadi ya imani, kwa kushirikishina mwanga wa upendo, mshikamano
na udugu, kama alivyosema Baba Mtakatifu Francisko katika hotuba yake alipowasili
nchini Brazil.
Kardinali Bertone, anawachangamotisha wadau mbali mbali kusikiliza
kwa makini yale yatakayozungumzwa wakati wa Maadhimisho ya Siku ya Vijana Duniani
ili hatimaye, waweze kuyamwilisha katika uhalisia wa maisha yao.