Baba Mtakatifu Francisko mara baada ya kuwasili nchini Brazil tayari kwa Maadhimisho
ya Siku ya 28 ya Vijana Duniani kwa Mwaka 2013 inayoongozwa na kauli mbiu, "Basi enendeni,
mkawafanye mataifa yote kuwa ni wanafunzi", anawaambia vijana kwamba, ule wakati waliokuwa
wanausubiri, umewadia, tayari wameenza juma la kujenga na kukuza urafiki wao na Yesu
Kristo.