2013-07-20 11:37:40

Papa Francisko na Baba Mtakatifu mstaafu Benedikto XV1 pamoja waombea Mkutano wa 28 wa Vijana Rio.


Ijumaa zikiwa zimebaki siku tatu kabla ya kufanya ziara yake ya kwanza ya Kitume ya Kimataifa, kutembelea Rio de Janeiro Brazil, Papa Francisko, kwa moyo wa upendo na uungwana namshikamano wa karibu na mtagulizi wake, alikwenda kumtembelea Mstaafu, Papa Benedikto XV1, katika monesteri ya Vatican, kumwomba aongozane nae kiroho katika ziara hii aliyoiitisha yeye Papa Ratzinger.
Maelfu ya vijana wanaendelea kukusanyika Rio de Janeiro, kwa ajili ya maadhimisho 28 ya Siku ya Vijana ya Dunia, na Papa Francisko atakwenda kuungana nao siku Jumatatu hii 22 Julai 2013.
Ijumaa, Papa Benedict XVI na Francisko walipokutana walipata muda wa nusu saa wa kusali pamoja, wakiombea tukio hili la WYD na walishirikishana mawazo juu ya tukio hili. Papa Francisko pamoja nae alikuwa na medali maalum aliyoiandaa kama kumbukumbu ya safari na pia alikuwa na kijitabu kidogo , vitu alivyo mzawadia Mstaafu Papa Benedict XVI, ambaye alisema kwa hakika vitamkumbusha kutolea sala zake na kuwa nae karibu kiroho wakati wote na hasa katika siku zote za tukio hili, linalo mkumbusha maadhmisho aliyoyashiriki huko Cologne, Sydney na Madrid.
Papa Francisko, Jumatatu 22 Julai 2013, majira ya saa tatu, ataanza safari ya kuelekea Rio de Janeiro, ambako kwa muda wa wiki zima ataungana na Vijana kwa ajili ya Maadhimisho ya 28 ya Siku ya Vijana ya Dunia. Papa anakwenda kukutana na vijana kwa lengo la kuwaimarisha kiroho, kama inavyotaja madambiu kwa adhimisho – “Nendeni mkawafanye wote kuwa wanafunzi wangu”. Hivyo ni maadhimisho ya kuitangza Injili ya Upendo wa Yesu wa kuokoa. Katika sherehe hizi, akti ya mambo mengine Papa ataongoza Ibada za misa, njia ya Msalaba na Mkesha wa sala.







All the contents on this site are copyrighted ©.