2013-07-17 11:15:51

"Mandela Day; Miaka 95 si haba!


Tarehe 18 Julai 2013 Mzee Madiba anatarajiwa kuadhimisha kumbu kumbu ya miaka 95 tangu alipozaliwa. Familia ya Mzee Nelson Mandela inasema kwamba, kwa vile Mzee Madiba hali yake bado ni tete tangu alipolazwa Hospitalini takribani mwezi mmoja uliopita hawatakuwa na maadhimisho ya kukata na shoka!

Siku ya Nelson Mandela itaadhimishwa nchini Afrika ya Kusini na sehemu mbali mbali duniani ili kukumbuka mchango mkubwa uliotolewa na Mzee Madiba katika mapambano dhidi ya sera za ubaguzi wa rangi Afrika ya Kusini. Umoja wa Mataifa, kunako mwaka 2009 ulitangaza kwamba, tarehe 18 Julai ya kila Mwaka itakuwa ni Siku ya Mandela. Mwaka huu "Mandela Day" Inaadhimishwa wakati ambapo Mzee Madiba anaendelea kupambana na mauti!

Katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa Bwana Ban Ki-Moon anapenda kutoa mwaliko kwa Jumuiya ya Kimataifa, kuhakikisha kwamba, inafanya kumbu kumbu kama njia ya kuendelea kumuenzi Mzee Madiba, kutokana na mchango wake, uliopelekea maboresho makubwa si tu nchini Afrika ya Kusini, bali duniani kote!







All the contents on this site are copyrighted ©.