2013-07-17 10:26:22

Mali kuingia kwenye kinyang'anyiro cha uchaguzi mkuu hapo tarehe 28 Julai 2013, lakini kampeni zimedorora!


Katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa Bwana Ban Ki-Moon, amewataka wanasiasa nchini Mali kuhakikisha kwamba, uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika nchini humo hapo tarehe 28 Julai 2013 unakuwa huru na wa haki na kwamba, wanasiasa wakubali pia matokeo.

Jumuiya ya Kimataifa inaendelea kufuatilia kwa ukaribu mchakato wa uchaguzi mkuu ili kufunga kipindi cha serikali ya mpito, iliyoingia madarakani kunako mwezi Mei, 2012 baada ya Serikali iliyokuwa imechaguliwa kihalali kupinduliwa kutoka madarakani.

Wachunguzi wa mambo wanasema, kwa sasa kampeni bado hazijaanza kushika kasi ya kutosha licha ya muda kuzidi kuyoyoma kwa kasi. Hii inachangiwa pengine na Mfungo Mtukufu wa Mwezi Ramadhani, kwani asilimia 90% ya wananchi wa Mali ni waamini wa dini ya Kiislam. Kuna jumla ya wanasiasa 28 wanaowania kuchaguliwa kuongoza Mali kama Marais.







All the contents on this site are copyrighted ©.