China ni kati ya wadau wakuu wa biashara nchini Angola ambayo katika kipindi cha miaka
ya hivi karibuni, biashara kati ya nchi hizi mbili imeongezeka maradufu, kiasi cha
kufikia dolla za kimarekani billioni tatu, ambayo ni asilimia 43% ya biashara yote
kutoka China.
Taarifa zinaonesha kwamba, Angola imeuza bidhaa zake nchini
China na kupata kiasi cha billioni 2.5, ambacho ni asilimia 11% ya bidhaa zote zilizoagizwa
na China kutoka Angola. China imewekeza kwa kiasi kikubwa nchini Angola katika sekta
ya ujenzi, vifaa vya umeme na nguo kiasi cha kutawala soko la Angola ambalo lina mvuto
mkubwa kutoka sehemu mbali mbali za dunia.