2013-07-13 07:59:51

Upendo na huruma vinavyomwilishwa katika huduma: kiroho na kimwili


Shirika la Masista wa Upendo la Huruma wa Mtakatifu Vincent wa Paulo, Mitundu, Singida, Tanzania linalojiandaa kuwa ni Kanda kamili panapo majaliwa mwishoni mwa Mwaka 2013, hivi karibuni, limemwimbia Mwenyezi Mungu utenzi wa sifa na shukrani kwa kuwajalia kupata watawa wapya tisa, kati yao nane walifunga nadhiri za kwanza na mtawa mmoja alifunga nadhiri zake za daima. RealAudioMP3

Ibada ya Misa Takatifu iliyoongozwa na Mheshimiwa Padre Francis Lyimu, msaidizi wa Askofu msimamizi wa kitume wa Jimbo Katoliki Singida na kupokelewa na Sr. Verediana Herman, Mama Mkuu wa Kanda. Hadi sasa Shirika la Masista wa Upendo la Huruma wa Mtakatifu Vincent wa Paulo, Mitundu linatekeleza dhamana na wajibu wake wa kichungaji katika Majimbo ya Singida, Mbeya, Kigoma na Jimbo kuu la Dar es Salaam.

Wamejikita katika utoaji wa huduma ya afya, elimu na maendeleo endelevu yanayotafsiriwa kwa namna ya pekee katika matendo ya huruma: kiroho na kimwili. Masista hawa wanaongozwa na fadhila za Mtakatifu Vincent wa Paulo, yaani kuwahudumia na kuwainjilisha maskini. Masista hawa wanaongozwa na roho ya shirika inayowasukuma kuonesha moyo wa unyenyekevu, unyofu, upendo na huruma.

Utume huu unajielekeza zaidi katika kumfuasa Kristo aliyejitoa bila ya kujibakiza kwa ajili ya kuwatangazia maskini Habari Njema ya Wokovu; kuishi na kumwilsiha kanuni ya maisha; kuonesha upendo na ibada kwa mwenyezi Mungu kwa njia ya huruma kwa maskini pamoja na kuishi fadhila zinazoongoza maisha na utume wao: unyenyekevu, unyofu, upole, kujitiisha kwa hiyari kwa ajili ya wokovu wa watu.









All the contents on this site are copyrighted ©.