Jumapili tarehe 14 Julai 2013, Papa kuongoza Sala ya Malaika wa Bwana, Ikulu Ndogo
ya Castel Gandolfo
Baba Mtakatifu Francisko, Jumapili tarehe 14 Julai 2013 anatarajiwa kuongoza Sala
ya Malaika wa Bwana, akiwa kwenye Ikulu Ndogo ya Castel Gandolfo, nje kidogo ya mji
wa Roma. Akiwa Castel Gandolfo, Baba Mtakatifu atatumia fursa hii kukutana na kuzungumza
na wafanyakazi wa Ikulu Ndogo ya Castel Gandolfo ambayo hutumika kwa ajili ya mapumziko
ya Papa wakati wa Kipindi cha Joto.
Hii itakuwa ni nafasi kwa Baba Mtakatifu
kukutana na kuzungumza pia na viongozi wa Kanisa na Serikali wa Mji wa Castel Gandolfo.
Hii itakuwa ni mara ya pili kwa Baba Mtakatifu Francisko kutembelea Castel Gandolfo,
tangu alipochaguliwa kuliongoza Kanisa kama Khalifa wa Mtakatifu Petro. Mara ya kwanza
ni wakati ule alipokwenda kumtembelea na kusali na Baba Mtakatifu mstaafu Benedikto
wa kumi na sita, tukio la kihistoria ambalo limeacha kumbu kumbu katika mioyo ya waamini
wengi hapo tarehe 23 Marchi 2013.