2013-07-06 15:16:45

Ukristu hauna muda bali ni kila wakati


Kuwa Mkristo haihitaji kufanya mengi , bali ni kuruhusu kufanywa upya na Roho Mtakatifu. Ni msisitizo wa Papa Francisko wakati wa Ibada ya Misa mapema Jumamosi , ibada aliyo iongoza katika Kanisa dogo la Mtaktifu Marta la mjini Vatican, ikiw ani ibada yake ya mwisho kabla ya mapumziko ya kipindi cha majira ya joto Ulaya, baada ya kuwa na mfululizo wa Ibada zake za asubuhi alizo ziongoza katika kanisa dogo la Mtakatifu Marta tangu achaguliwe kuwa Papa. Katika Ibada hiyo ya Jumamosi pia alisema , hata katika maisha ya kanisa, kuna miundo ya kale, bila shaka inayohitaji kufanywa upya . Miongoni mwa waliohudhuria Ibada hiyo ni pamoja na kundi la Walinzi wa Kipapa, "The Uswiss Guards ".

Homilia ya Papa ililenga katika somo la Injili juu ya mfano wa Mvinyo mpya juu ya Mivinyo mingine, na alirejea utajiri wa mafundisho ya Yesu , juu ya sheria , akisema , Yesu alifanya mambo yote kuwa mapya. Na ulikuwa upya wa kweli katika sheria, kwa ajili ya kuiimarisha zaidi sheria iliyokuwepo. Na kwamba, hoja za Yesu kufanya mabadiliko mapya katika sheria, zilikuwa na nguvu zaidi kuliko sheria yenyewe ilivyokuwa. Papa alieleza na kutoa mfano wa sheria inahusu kumchukia adui, badala yake Yesu anasema mwombee mema adui yako. Kumbe basi, hii inamaanisha Yesu alikuwa akihubiri sheria za kuufikia Ufalme wa Mungu,kwa kufanya mabadiliko katika maisha kwa kuanzia ndani ya mioyo yetu.
Papa alieleza na kuonya dhidi ya kufikiri kwamba, njia ya Kikristo ni kufanya hiki na kile. . La sivyo. Kuwa Mkristo ina maanisha kuruhusu kufanywa wapya na Yesu katika njia yake mpya ya maisha. Na haitoshi kusema , Mimi ni Mkristo mzuri, kila Jumapili, na nashiriki Ibada ya Misa. Pengine tunafanya hivyo kama mazoea tu ya kila Jumapili, kumbe ndani mwetu mna imani haba na matendo yetu hayazingatii mafundisho ya Yesu. Papa ameasa maisha ya Kikristu hayafungamanishwi na mambo ya kidunia lakini ni maisha yanayoongozwa na Roho Mtakatifu kila wakati , akitufanya wapya katika kuishi na wenzetu . Na haiwezekani kuyachukua maisha hayo katika mfumo wa vipande vipande na kuacha menginena Ukristu hauna muda. Wakati wote ni sawa katika mwenendo wake.. na kuwa Mkristo haina maana mwisho wa maisha ya furaha lakini ni daima ni kama mwanzo wa furaha ya kufanywa upya na Roho Mtakatifu, au kwa kutumia maneno ya Yesu, kuwa divai mpya."









All the contents on this site are copyrighted ©.