Rais Carmona akutana na kuzungumza na Papa Francisko mjini Vatican
Baba Mtakatifu Francisko, Jumamosi, tarehe 6 Julai 2013 amekutana na kufanya mazungumzo
na Bwana Anthony Thomas Aquinas Carmona wa Jamhuri ya Trinidad na Tobago.
Rais
Carmona baadaye alikutana na Kardinali Tarcisio Bertone, Katibu mkuu wa Vatican aliyekuwa
ameandamana na Askofu mkuu Dominique Mamberti, Katibu mkuu wa mambo ya nchi za nje
na ushirikiano wa kimataifa mjini Vatican.
Katika mazungumzo yao, viongozi
hawa wawili wamegusia kuhusu mchango wa Kanisa Katoliki naotolewa kwa wananchi wa
Trinidad na Tobago hasa katika sekta ya elimu, afya na huduma kwa maskini na wale
wanaosukumizwa pembezoni mwa Jamii. Ni matumaini ya viongozi hawa wawili kwamba, ushirikiano
baina ya pande hizi mbili utaendelezwa kwa ajili ya mafao ya wengi.
Viongozi
hawa wameguswa na matatizo yanayowakabili vijana hasa katika mapambano dhidi ya makosa
ya jinai. Kwa pamoja wamekazia umuhimu wa majiundo kwa ajili ya mtu mzima: kiroho
na kimwili pamoja na kulinda mazingira kwa ajili ya ustawi na maendeleo ya wengi.