2013-07-04 13:59:05

Waziri mkuu wa Italia Bwana Enrico Letta akutana na kuzungumza na Papa Francisko!


Baba Mtakatifu Francisko, Alhamisi, 4 Julai 2013 amekutana na kuzungumza na Waziri mkuu wa Italia Bwana Enrico Letta. Baada ya kuzungumza na Baba Mtakatifu, Waziri mkuu alipata fursa ya kukutana na kuzungumza na Kardinali Tarcisio Bertone, Katibu mkuu wa Vatican pamoja na Askofu mkuu Dominique Mamberti, Katibu mkuu wa mambo ya nchi za nje na ushirikiano wa kimataifa mjini Vatican.

Viongozi hawa wawili katika mazungumzo yao, wamegusia kwa namna ya pekee, changamoto zinazoikabili Italia na nchi za Ulaya katika ujumla wake pamoja na kuibua mbinu mkakati utakaoziwezesha nchi hizi kulinda fursa za ajira hasa miongoni mwa vijana. Wamejadili kuhusu uhusiano uliopo kati ya Familia za Wananchi wa Italia na Kanisa Katoliki katika ujumla wake na changamoto ya kuendelea kudumisha amani na utulivu.

Baba Mtakatifu na Waziri mkuu wa Italia, wamejadili pamoja na mambo mengine pia kuhusu masuala ya kimataifa sanjari na mageuzi yanayoendelea kujitokeza sehemu mbali mbali za dunia. Kwa pamoja wamekubaliana kwamba, kuna haja kwa wadau mbali mbali nchini Italia kuendelea kushirikiana kwa ajili ya ustawi na maendeleo ya wananchi wa Italia katika ujumla wake na kwa ajili ya mafao ya Jumuiya ya Kimataifa.







All the contents on this site are copyrighted ©.