2013-07-04 12:13:15

Watetezi wa haki msingi za binadamu waomba adhabu ya kifo isitishwe nchini Nigeria


Taarifa kutoka nchini Nigeria zinaonesha kwamba, kuna jumla ya wafungwa 1,000 wanaosubiri utekelezaji wa hukumu ya kifo. Hawa ni wale waliohukumiwa adhabu hii na utawala uliopita. Kutokana na taarifa hii, Tume ya haki ya Umoja wa Afrika imeiomba Serikali ya Nigeria kusitisha utekelezaji wa adhabu ya kifo, baada ya wafungwa wanne waliohukumiwa adhabu hii kunyongwa hivi karibuni, hali ambayo iliibua shutuma kutoka ndani na nje ya Nigeria.

Wafungwa hao walinyongwa mara baada ya Rais Goodluck Jonathan wa Nigeria kutia sahihi hati ya kunyongwa kwa wafungwa watano, mmoja bado anasubiri utekelezaji wa adhabu hii. Mwanasheria na mtetezi wa haki msingi za binadamu Femi Falana ametuma ombi kwa niaba ya watetezi wa haki msingi za binadamu kutoka Nigeria ili kusitisha adhabu ya kifo inayowakabili wafungwa wengine magerezani.







All the contents on this site are copyrighted ©.