2013-07-03 15:07:02

Mshikamano wa Vatican na wananchi wa Afrika ya Kati


Kardinali Fernando Filoni, Msimamizi wa Baraza la Kipapa kwa ajili ya Uinjilishaji wa Watu, mapema Jumatatu alimpokea , Askofu Mkuu Dieudonné Nzapalainga wa Jimbo Kuu la Bangui, akiwa amefuatana na kundi la la waamini ishirini, waliomsindikiza katika Ibada ya kuvalishwa Palium na Papa Fransisko.
Ibada iliyofanyika Jumamosi Juni 29 katika Kanisa Kuu la Mtakatifu Petro, ikienda sambamba na Siku Kuu ya Kiliturujia ya Watakatifu Petro na Paulo .
Kwa mujibu wa taarifa ya fides, baada ya mkutano wa faragha na Askofu Mkuu Nzapalainga, Kardinali Filoni alikutana pia wa kundi la waamini. Katika hotuba yake aliwatia moyo dhidi ya hali ngumu ya maisha kama kanisa, yanayopita katika kipindi hiki hasa baada ya kuangushwa kwa utawala wa Rais Bozize. Alitaja ukaribu kiroho na mshikamano unaoonyeshwa na Shirika la Kipapa kwa ajili ya Uenezaji imani, kwa watu nzima katika Afrika ya kati, na matumaini ya baadaye yake katika upatikanaji wa amani ya kudumu.
Kardinali alikumbuka pia ziara yake ya kichungaji aliyoifanya mwaka jana Julai Afrika ya Kati, ambako aliwaweka Wakfu Maaskofu wapya wanne, ikiwa ni pamoja na Askofu Mkuu wa Bangui. Kardinali alisisitiza kwamba Kanisa katika Jamhuri ya Afrika ni kati ya maeneo yanayotazamwa kwa makini na Shirika kwa ajili ya Uinjilishaji wa watu, na linakusudia kuendelea kusaidia ukuaji wa kanisa na kukufanya upya kwa ajili ya kufanikisha ukomavu zaidi.
Na kwa niaba ya waamini, Godefroy Mokamanede Francis alimshukuru Papa kwa maombi na baraka zake kwa ajili ya neema ya Jamhuri ya Afrika ya Kati, aliyoyatoa wakati wa sala ya Malaika wa Mbingu , Jumamosi Juni 29. Na pia alitoa shukurani kwa Kardinali Filoni , kwa kuwa na nafasi ya kukutana nao. Katika hotuba yake, hakusahau kutoa sauti ya kilio cha watu wa CAR, ambao kwa wakati huu wanapambana na hali ngumu halisi za jamii kutojali maadili ya maisha iwe kijamii, kisiasa na kidini pia , hali inayowatia watu wenye mapenzi hofu na wasiwasi juuya mustakabhali wa jamii na maslahi mengine katika taifa hilo.
Kardinali akiagana na ugeni huo, aliwahakikishia wao si peke yao. Kanisa lote ni pamoja nao. Kisha aliwahimiza daima kuwa wajenzi wa amani na haki. Na aliwazawadia wote, Rosari iliyobarikiwa na Baba Mtakatifu akiwaomba watoleee maombi yao kwa Mama Yetu wa Afrika, na wafikishe baraka la Papa walizopokea kwa waaamini wote , huku akionyesha tumaini kwamba watakutana tena siku zijazo.









All the contents on this site are copyrighted ©.