2013-07-02 11:32:59

Wake wa Marais wa Marekani wapania kuwajengea uwezo wanawake wa Afrika!


Mama Michelle Obama na Mama Laura George Bush wa Marekani, wameamua kuunganisha nguvu zao ili kuwekeza kwa wanawake Barani Afrika, ili kuwajengea uwezo wa kiuchumi pamoja na kupambana fika na changamoto za maisha.

Hizi ni juhudi ambazo zinafanywa kwa mara ya kwanza na wanawake wa Marais hawa wawili wa Marekani, kama sehemu ya mchakato wa kuendeleza mafanikio yaliyopatikana chini ya uongozi wa Rais George W. Bush wa Marekani hasa kampeni dhidi ya ugonjwa wa Ukimwi Barani Afrika. Uamuzi huo umefikiwa na wanawake wa Marais wa Marekani muda mfupi tu kabla ya kufanya kumbu kumbu kwa watu walioathirika kutokana na vitendo vya kigaidi kwenye Ubalozi wa Marekani, Jijini Dar es Salaam kunako mwaka 1998.

Mfuko wa Bush unasaidia sana katika mchakato wa maboresho ya afya ya wanawake Kusini mwa Jangwa na Sahara na katika Nchi za Amerika ya Kusini.







All the contents on this site are copyrighted ©.