Baba Mtakatifu Francisko kwa Mwezi wote wa Agosti, hataweza kutoa Katekesi zake kwa
Siku ya Jumatano hadi tarehe 4 Septemba 2013. Katika mwezi Agosti, Baba Mtakatifu
ataendelea kusali na waamini pamoja na mahujaji watakaofika kwenye Uwanja wa Kanisa
kuu la Mtakatifu Petro, mjini Vatican.
Taarifa inaonesha kwamba, Baba Mtakatifu
tarehe 15 Agosti 2013, katika Maadhimisho ya Siku kuu ya Bikira Maria Kupalizwa Mbinguni,
ataadhimisha Ibada ya Misa Takatifu kwenye Ikulu Ndogo ya Castel Gandolfo, nje kidogo
ya mji wa Roma, baadaye, atasali pamoja na waamini Sala ya Malaika wa Bwana. Idhaa
ya Kiswahili ya Radio Vatican itaendelea kukujuza yale yatakayokuwa yanajiri mjini
Vatican na sehemu mbali mbali za dunia! Waswahili wanasema, "Stay Tuned".