2013-07-02 15:31:10

Mkurugenzi na Naibu wake, wamejiuzuru IOR


Tamko kutoka Ofisi ya Habari ya Vatican juu ya yanayoendelea katika Idara ya Fedha ya Vatican (IOR), linaeleza kwamba, aliyekuwa Mkurugenzi wa IOR, Paolo Cipriani na Naibu Mkurugenzi Massimo Tulli wametoa hati za kujiuzuru kutoka nafasi zao, baada ya utumishi wa muda mrefu. Wametaja sababu za kujiuzuru kwao kwamba, ni kwa manufaa ya Taasisi hiyo na Jimbo Takatifu.

Baraza la Usimamizi la tume hiyo na Tume ya Makardinali inayohusika na masula ya fedha na uchumi wa Vatican, wamekubali kujiuzulu kwao. Vivyo hivyo tume iliyoteuliwa hivi karibuni na Papa , imekubali uamuzi huo. Katika nafasi zao wameteuliwa Rais waTume Ernst von Freyberg, kuwa pia Mkurugenzi Mkuu wa Muda, kazi anayoianza mara moja, na jopo la udhibiti la AIF Vatican, limekubali taarifa hiyo.

Ernst Freyberg von atatenda kwa kusaidiana na Rolando Marranci kama kaimu Naibu Mkurugenzi na Antonio Montaresi anachukua nafasi ya Afisa Mkuu wa Tahadhari, na msimamizi wa miradi maalum. Hapo awali Rolando Marranci aliwahi kuwa Afisa Uendeshaji Mkuu katika benki moja ya Italy iliyoko London. Na Antonio Montaresi aliwahi kuwa msimamizi na Afisa Mkuu wa Mwafaka na benki mbalimbali nchini Marekani.
Taasisi ya Fedha ya Vatican , IOR, ilianzishwa mwaka 1942 kwa maamuzi ya Papa . Madhumuni ya IOR ni kuhudumia Jimbo Takatifu na Kanisa Katoliki duniani kote, kama inavyoelezwa katika Katiba yake. IOR hutunza mali za vikundi , taasisi na mashirika yenye kutambulika kisheria na yenye kuhusiana na Kanisa la Katoliki kama inavyoelezwa kisheria na Vatican. IOR, ina wafanyakazi 114, na ni peke ambayo ofisi zake zilijengwa ndani ya nchi ya Vatican.







All the contents on this site are copyrighted ©.