2013-07-02 16:14:25

Mkristu anatakiwa kubaki shujaa licha ya udhaifu wake


Wakristu wametakiwa kubaki imara katika imani na kuachana na hofu na woga wa kuachana na dhambi. Wanatakiwa kuwa jasiri katika kupambana na mawimbi ya majaribu ya dhambi yanayo taka kuudhoofisha moyo.Ni wito wa Papa Fransisko, wakati akiongoza Ibada ya Misa, mapema Jumanne katika kanisa dogo la Mtakatifu Marta ndani ya Vatican.

Papa amesema kwamba, tunapaswa kutambua kwamba, sisi ni dhaifu na hivyo ni lazima kuikimbia dhambi bila kutazama mazoea mabaya ya nyuma. Katika Ibada hiyo , Papa aliiongoza akisadiana na Kardinali Manuel Monteiro de Castro, na Mapadre Kadhaa. Pia ilihudhuriwa na Walei wafanyakazi wa Mahakama ya Kitume ya Kitubio na kundi jingine kutoka la Chuo cha Kipapa cha Kikanisa.


Katika homilia yake Papa alitafakari juu ya masomo ya siku , akiangalisha katika mapambano ya kiroho dhidi ya dhambi , na kuainisha mambo manne katika masomo hayo kwamba , kuna utendaji wa kutenda polepole, kuna kuyaangalia ya nyuma, kuwa na hofu na kurejea kwa Bwana kwa neema ya Roho Mtakatifu.

Papa Fransis, ameyaangalia hao katika mtazamo wa uwezekanavyo wa kujikwamua na mapambano ya kiroho na matatizo mengine. Papa alianza kwa kutazama tabia ya kutenda polepole katika kuyaacha ya nyuma, kama ilivyokuwa kwa Lutu aliyeamuriwa kuondoka katika mji kabla haujaharibiwa , lakini akafanya hivyo polepole kwa kinyongo. Malaika anamharakisha kukimbia, lakini yeye ndani yake hana uwezo huo wa kukimbia kutoka uovu na dhambi, kwa kuwa ana yatamani ya nyuma yanayoangamiza. Na ndivyo ilivyo hata kwetu leo hii, tunatakiwa kwenda nje ya dhambi , lakini tunapata kigugumizi kuamua hivyo, kwa kuwa tunayatamani yale yanayoangamiza, tunavutwa nyuma badala ya kwenda mbele, kama ilivyokuwa katika majadiliano kati ya Malaika na Lutu.

Papa anasema ni jinsi gani ilivyokuwa vigumu kujitenga na dhambi. Ni vingumu pia kushinda majaribu , lakini Sauti ya Mungu inatuambia katika neno lake , kimbia, huwezi kupambana na moto wa dhambi wenye kukuua. Pia Mtakatifu Tereza wa Mtoto Yesu, alifundisha, wakati mwingine, katika majaribu , suluhu pekee ni kutafuta namna ya kutoroka. Hakuna sababu za kuonea aibu kutoroka. kutoroka niujasiri, ni kutambua kwamba, sisi ni dhaifu na hivyo inabidi kutoroka kabla dhambi haijatumaliza. Na mahali pekee pa kutorokea ni katika njia ya Yesu.

Papa alieleza na kukemea udhaifu wa kuyatazama ya nyuma kama alivyofanya Lutu. Na ametaja njia inayofaa kumaliza hamu ya kurudia dhambi , kukumbuka vinono vya kulaghai vilivyowekwa juu ya meza ya dhambi, na mauti, ni kuukaza uso kwa Bwana, na kusema, sirudi nyuma. Ni kutazama ya mbele tu na kupiga hatua katika mwendo huo bila ya kuyafikiri yaliyopita.

Papa amekiri udhaifu wa binadamu akisema sisi sote ni dhaifu , na hivyo, kwa utambuzi huo, ni lazima kuwa na ujasiri wa kujilinda dhidi ya udhaifu huo. Kwa namna gani ni kukimbilia msaada wa Bwana na kumwambia , Bwana nina zama, niokoe, kama ilivyokuwa kwa wanafunzi wa Yesu, walipopigwa na mawimbi makali baharini , walimwamsha Bwana na kusema Bwana tuokoe tunaangamia. Walikuwa na hofu. Na hofu hiyo ni majaribu ya shetani, ni kuwa na hofu ya kusonga mbele katika njia ya Bwana.

Papa anasema, kuna majaribu mengi , kama ilivyokuwa kwa wana wa Israel wakati wa kukombolewa katika utumwa , walifika mahali wakasema, heri utumwa wa Misri. Walishikwa na hofu za kusonga mbele. Ni woga na kukata tamaa.


Papa amewatia shime Wakristu akisema, hakuna sababu ya kuongoza au kukata tamaa. Lete hofu zako zote kwa Yesu anayewaaambia wafuasi wake , msiogope. Msiogpe hofu haina msaada kwetu. Msaada wetu, ni neema ya Roho Mtakatifu.


Papa ameonya daima, kabla ya dhambi kutenda dhambi na mbele ya hamu ya kutenda dhambi, huwa kuna hofu fulani inayoonya, usipoteze nafasi hiyo, wahi kw akutafuta msaada wa Bwana, mwite nayemara moja atakujibu. Sema Bwana naangamia, nae atakusadia.


Na kwamba kweli sisi sote ni dhaifu, lakini ni lazima tuwe jasiri kupambana na udhaifu huo. Na ujasiri wetu hupata nguvu kwa kukataa kutazama ya nyuma, ni kuyakimbia, na wala tusikubali kuzama katika hamu za mambo ya nyuma au mazoea mabaya. "Usiogope, daima kaza uso wako kwa Bwana! "








All the contents on this site are copyrighted ©.