Waraka wa kwanza Kitume wa Papa Fransisko kuwasilisha Ijumaa wiki hii
Waraka wa kwanza wa Kitume wa Papa Fransisko ni juu ya Mwanga wa Waamini( Lumen
Fidei) Mkuu wa Dekania ya Maaskofu Kardinali Marc Oullet , Askofu MKuu Gerhard
Ludwig Muller, na Mkuu wa Shirika kwa ajili ya Mafundisho Sadikifu na Mkuu wa Baraza
la Kipapa kwa ajili ya Ukuzaji wa Uinjlishaji mpya Askofu Mkuu Rono Fischella, Ijumaa
ijayo watawasilisha Waraka wa Kwanza wa Kitume, Papa Fransisko, mbele ya Wanahabari.
Waraka wenye jina Lumen Fidei. Wanahabri wote wenye dhamana Vatican mnaalikwa kufika
katika ukumbi wa Yohane Paulo 11 wa Ofisi ya Habari ya Vatican, majira ya saa sita
kamili , Ijumaa tarehe 5 Julai 2013. . Waraka huo umeandikwa katika lugha ya
Kiitaliano, Kiingereza Kifaransa , Kijeruman, Kihispania na kireno pia.