Familia ya Mzee Madiba yakutana na Rais Obama na Mkewe!
Rais Barack Obama wa Marekani katika ziara yake ya kikazi nchini Afrika ya Kusini,
Jumamosi tarehe 29 Juni 2013 alikutana kwa faragha na familia ya Rais mstaafu Nelson
Mandela na kuzungumza nayo! Mkutano huu wa faragha umefanyika kwenye kituo cha Mfuko
wa kumbu kumbu ya Nelson Mandela. Mazungumzo haya yamedumu kwa takribani nusu saa
kadiri ya taarifa kutoka Ikulu ya Marekani.