Monsinyo Nunzio Scarano amesimamishwa kazi kwa uchunguzi!
Padre Federico Lombardi msemaji mkuu wa Vatican anasema, Vatican inasubiri taarifa
rasmi kuhusu kukamatwa kwa Monsinyo Nunzio Scarano anayetuhumiwa kujihusisha na mchakato
wa utakatishaji wa fedha chafu. Kwa takribani mwezi mmoja uliopita, Nunzio Scarano
ambaye alikuwa anafanya kazi katika Idara ya fedha (APSA) mjini Vatican alisimamishwa
kazi kwa uchunguzi.
Vatican imeonesha utayari wa kushirikiana na Serikali
ya Italia ili kupata ukweli wa tukio hili. Wakati huo huo, Vatican AIF inaendelea
kuchunguza tukio hili kama itabidi kuchukua hatua stahiki!