Papa Francisko ni kati ya viongozi mashuhuri wanaoendelea kuitikisa dunia kwa sasa!
Utafiti uliofanywa na Shirika la Habari la Adnkronos na kuchapishwa katika kitabu
chenye kurasa 960, unaonesha kwamba, Baba Mtakatifu Francisko ni kati ya watu mashuhuri
walioitikisa dunia katika kipindi cha Mwaka 2013. Kitabu hiki ambacho kiko tayari
mitaani, kina ujumbe muhimu uliotolewa na Baba Mtakatifu Francisko kwa wakuu wa Serikali
na Jumuiya ya Kimataifa katika medani mbali mbali za maisha pamoja na watu wenye mapenzi
mema.
Baba Mtakatifu anawataka viongozi hao kuhakikisha kuwa, wanatunza mazingira,
kielelezo cha mpango wa Mungu ulioandikwa katika mazingira na kwamba, wanapaswa kuwa
ni walinzi kwa jirani zao. Hii ni changamoto ya kujikita katika maendeleo endelevu!