2013-06-27 10:35:29

Kikosi cha waasi wa Seleka wataingamiza nchi!


Jamhuri ya Afrika ya Kati ni taifa ambalo linaendelea kupoteza dira na mwelekeo wa maisha, kiasi kwamba, ile misingi ya haki, amani, umoja, upendo na mshikamano wa kitaifa vinatoweka taratibu kutokana na vita inayoendeshwa na Kikosi cha Waasi wa Seleka, baada ya mapinduzi ya Serikali yaliyofanyika kunako tarehe 24 Machi 2013.

Hayo yamebainishwa na Askofu mkuu Diudonnè Nzapalainga, wa Jimbo kuu la Bangui. Kikosi cha Waasi wa Seleka kimekuwa kikiendelesha madhulumu ya kidini dhidi ya Wakristo pamoja na kusababisha watu kukimbia maeneo yao kutokana na kukosekana kwa misingi ya haki, amani na utulivu. Hii ni changamoto kwa viongozi mbali mbali wa kisiasa na kidini kukaa pamoja ili kujadili hatima ya maisha ya wanachi wa Jamhuri ya Afrika ya Kati.







All the contents on this site are copyrighted ©.