Waziri mkuu wa Italia kukutana na Papa Francisko hapo tarehe 4 Julai 2013
Waziri mkuu wa Italia Bwana Enrico Letta anatarajiwa Alhamisi, tarehe 4 Julai 2013
kukutana kwa faragha na kuzungumza na Baba Mtakatifu Francisko na baadaye atakutana
na kuzungumza pia na Kardinali Tarcisio Bertone, Katibu mkuu wa Vatican. Hayo yamebainishwa
na Padre Federico Lombardi, msemaji mkuu wa Vatican.